Jumatano 21 Mei 2025 - 08:45
Huduma za Shahidi Raisi zilikuwa chanzo cha heshima ya kitaifa, izza ya taifa, na itibari ya wananchi wa Iran / Wamarekani waache upayukaji; Iran haitasubiri ruhusa ya mtu yeyote kwa ajili ya urutubishaji wa nyuklia

Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, asubuhi ya jana, katika kikao na familia ya Shahidi Raisi na mashahidi wengine, pamoja na familia za mashahidi waliokuwa na nyadhifa za juu katika miongo ya hivi karibuni, alieleza kuwa lengo kuu la kuwatukuza na kuwasifu mashahidi ni tafakuri na kujifunza kutoka kwao, huku akiainisha sifa alizo kuwa nazo Rais Shahidi moyoni, kimatamshi kimatendo, alisema: "Raisi mpenzi alikuwa mfano kamili wa sifa za mtu mwenye jukumu katika serikali ya Kimungu, na kwa jitihada zisizo na kuchoka alilitumikia taifa na heshima, izza, na itibari ya wananchi; njia na mtindo huu ni funzo kubwa kwetu sisi viongozi, kwa vijana na kwa vizazi vijavyo."

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Hawza, Ayatollah Khamenei vilevile, alitoa tanbihi kwa upande wa Marekani katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na, akasisitiza:
"Kauli za Wamarekani kuwa hawataruhusu Iran kufanya urutubishaji wa nyuklia ni upuuzi wa kiwango cha juu, na Jamhuri ya Kiislamu itaendeleza siasa na njia yake katika jambo hili bila kusubiri ruhusa ya mtu yeyote."

Hadhrat Ayatollah Khamenei alitaja kuwa lengo la upande wa pili kusisitiza juu ya mazungumzo ya moja kwa moja ni kuonesha taswira ya aina fulani ya kusalimu amri kwa Iran, na akasema:
"Shahidi Raisi hakuwapa nafasi hiyo. Bila shaka, katika zama zake, mazungumzo ya moja kwa moja hayakufanyika kama ilivyo sasa, na mazungumzo yaliyokuwepo yalikuwa yasiyo ya moja kwa moja, ambayo hayakufikia natija, na hivi sasa pia hatuoni uwezekano wa kupata natija, wala hatujui nini kitatokea."

Ayatollah Khamenei pia alitaja ripoti ya taasisi za kifedha za kimataifa kuhusu ongezeko la ukuaji wa uchumi wa Iran kutoka karibu asilimia sifuri mwanzoni mwa serikali ya kumi na tatu hadi karibu asilimia 5 mwishoni mwa kipindi hicho kuwa ni jambo la kujivunia, chanzo cha izza ya kitaifa na kiashirio cha maendeleo ya nchi, na akasema: "Kubeba Qur’an au picha ya Shahidi Soleimani katika kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ni miongoni mwa hatua nyingine alizochukua Shahidi Raisi ambazo kwa njia yake alilipa hadhi na heshima kubwa taifa la Iran.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha